Sunday, November 23, 2014

Serikali ya Kenya imesema kuwa imeanza kuwatambua waliotekeleza mauaji

Wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab waliwapiga risasi wasafiri ambao hawangeweza kukariri Koran.
Al Shabaab ilisema kuwa shambulizi hilo lilikuwa la kulipiza kisasi mauaji ya hivi majuzi ya waislamu yaliofanywa na wanajeshi wa Kenya kwenye mji wa pwani wa Mombasa.
Serikali ya Kenya imesema kuwa imeanza kuwatambua waliotekeleza mauaji hayo na itawafikisha mbele ya sheria hivi karibuni.
Mshauri wa ngazi ya juu wa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa mauaji ya watu 28 waliokuwa wakisafiri kwenye basi moja yalilenga kusababisha vita vya kidini nchini kenya.
Kwenye mahojiano na BBC Abdikadir Mohammed alitoa wito kwa wakenya kutoka imani zote kuungana pamoja dhidi ya kile alichokitaja kuwa vitendo vya uhalifu.

segerea iyooo mliozoea kuchezea watoto alafu mnatoweka sasa kimenuukaaa

Mkuu wa Wilaya ya Rufiji  Mkoani Pwani,Nurdin Babu  ameagiza wanafunzi24 wa Sekondari mbalimbali Wilayani humo waliopata ujauzito kuripoti kituo cha polisi November25 mwaka huu ili wasaidie kutoa ushirikiano wa kuwakamata wahusika waliowapa mimba na kuweze kukamatwa.
Sambamba  na wanafunzi hao pia wazazi au walezi wa wanafunzi hao  wametakiwa kuripoti wakiwa na watoto wao ambapo atazungumza na wazazi pamoja na wanafunzi hao ili kujua tatizo ni nini.
Babu alisema taarifa za watoto26 walipata ujauzito katika kipindi cha Januari hadi Oktoba si nzuri na lazima hatua za kinidhamu zichukuliwe ili kuondokana na matatizo hayo ndani ya jamii.
Alisema idadi ya wanafunzi waliokatishiwa masomo ni kubwa na Serikali haiwezi kulifumbia macho suala hilo

Wednesday, November 19, 2014

kumwagilia kinyesi kwenye mchicha

mboga za majani ni afya ila hii sasa inabidi wauzaji wae na dawa za magonjwa maana hii ni hatari kwa maisha ya mtumiaji mboga zinazolimwa  katika mazingira ya ajabu … sasa baraza la mazingira Tanzania NEMC limebaini kuwa wakulima wa mboga za majani wengi wamekuwa wakitumia majitaka kumwagilia hizi mboga.akisema na itv 
Afisa wa NEMC amezungumza  na kusema; “… Kama Serikali hatuwezi kuruhusu kitu kama hicho.. hatutaruhusu tena kumwagilia kinyesi kwenye mchicha, haturuhusu hicho kitu, hakuna serikali hiyo ambayo itaruhusu vitu hivi…

nald clever ft milker,single sally_shake your body

 come and shake your body toa barid its hot in herehttps://www.hulkshare.com/7gzm7fllrbb4

je tuseme zao walilolikataa askari sasa limeboreshwa na je mtazuia wadau kutumia maana m napaka mafuta wala si mvutaji

Familia ya aliyekuwa mwanamuziki wa Jamaica, Bob Marley imezindua kampuni ambayo wanaitaja kama ya kwanza duniani kuuza bidhaa za Canbbisa au marujuana au Bangi kama wanavyoijua wengi.
Bidhaa hizo zitajulikama kama 'Marley Natural' na na zitajumuisha mafuta ya urembo pamoja na manukato mengine ya wanawake na bidhaa nyinginezo.
Bidhaa hizo zitatengezwa na kampuni kubwa ijulikanano Privateer Holdings iliyo mjini Washington Marekani, ikisisitiza kutaka kudumisha kumbukumbu ya mwanamuziki huyo aliyesifika kote duniani.
Bidhaa hizo zitauzwa nchini Marekani na kwingineko duniani kunzia mwaka jana.
Mwanawe Bob Marley, Cedella Marley, alisema hayati babake angekuwa hai angefurahishwa sana na wazo hilo.
Bidhaa hizo zitakuwa za urembo kama vile mafuta na manukato
''Babangu angekuwa na fahari kubwa kuona watu wakitambua uwezo wa kuponya wa Bangi,'' alisema Cedella.
Mkuu wa kampuni hiyo, Brendan Kennedy alisema Marley alikuwa mtu ambaye kwa njia nyingi alisaidia kuanzisha harakati za kupinga juhudi za kuharamisha Bangi miaka 50 iliyopita.
"Marley alipenda sana kutumia Bangi na hakuna aliyemshinda kwa hilo duniani kote. ''
Bob Marley alifariki mwezi Mei mwaka 1981, kutokana na Saratani.Alipenda sana kutumia Bangi kama sehemu ya imani yake ya Rastafarian na kuunga mkono kuhalalishwa kwake.
Matumizi ya Bangi kwa ajili ya kujiburudisha yamehalalishwa katika majimbo ya Colorado na Washington nchini Marekani.
Majimbo mengine huenda yakaidhinisha matumizi ya Bangi nchini Marekani na mengine tayari yanaruhusu utumiaji wa bidhaa hiyo kwa sababu za matibabu.